26.Sep.2011 Nikki Mbishi @ TZhiphop.com
Wakati wimbo wake “Sauti ya Jogoo” ukiendelea kujaribu kuamsha Watanzania, bila shaka watu wengi wanataka kufahamu kitu gani hasa kilimsukuma Nikki Mbishi kuandika wimbo kama ule — mashairi mazito yaliyowasilishwa kwa utulivu na mpangilio wa hali ya juu.
Wakati anahojiwa na TZhiphop.com, Nikki alisema haya: “Nilikuwa nawaza kuongelea uhalisia wa tasnia ya siasa Tanzania inavyojenga matabaka — baina ya watu wa ‘chini’ na wa ‘juu’. Na pia nilitaka kuwakumbusha watu majukumu yao kama jogoo awaamshavyo waliolala alfajiri inapojiri.”
Zaidi ya hayo, Nikki aliongelea mambo mengine kuhusu kazi za kimuziki na ndoto zake baada ya miaka mitano. Mahojiano kamili yanapatikana hapa [bofya].
Pia, waandishi wa TZhiphop wamechambua nyimbo “Hisia” (Nikki, Stereo, Suma & One) na “Sauti ya Jogoo” (Nikki ft. Maulo na Bela Kombo). Makala zinapatikana [bofya]:





